MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA HANANG ASIMAMISHWA KAZI

Mkuu wa mkoa wa Manyara Dkt Joel Bendera ametangaza kumsimamisha kazi mkurugenzi wa halmashauri ya Hanang Bw Felex Mabula kutokana na tuhuma za ubadhirifu wa fedha  zaidi ya milioni 600 ambapo uamuzi huo umeutoa mbele ya watumishi pamoja na madiwani wa hlamshauri hiyo.

Dkt Joel Bendera ametangaza uamuzi huo wa kumsimamisha kazi Bw. Felex Mabula kutokana na tuhuma za ubadhirifu wa fedha zaidi ya milioni 600 ambapo ubadhirifu huo umeibuliwa na baraza la madiwani baada ya kupokea ripoti ya mkaguzi wa ndani wa halmshauri ya hii ya Hanang.

Nalo baraza la madiwani wa halmshauri hii ya Hanang kupitia mwenyekiti wake limesemakuwa halitakuwa tayari kutoa ushirikiano wa kikazi bw Mabula endapo uchunguzi utafanyika na kubaini kuwa msafi na kurejeshwa katika kiti chake.

Hata hivyo mkuu mkoa wa Manyara Dkt Joel Bendera baada ya kutangaza kumsimamisha kazi bw Mabula pia amemtaja Bw Werasare Munisi kuchukua nafasi ya mkurugenzi  huyu ambapo munisi alikuwa mhandisi wa maji halmashauri ya Hanang.
CHANZO CHANELTEN
SHARE

Unknown

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment