Uchaguzi wa majimbo ya Afrika Kusini utafanyika Agosti 3 mwaka huu.


Rais Jacob Zuma alitangaza tarehe hiyo siku moja tu baada ya kuponyoka kura ya kutokuwa na imani naye bungeni iliyokuwa ikiongozwa na vyama vya upinzani kufuatia kupatikana na hatia ya ubadhirifu wa mali ya umma na matumizi mabaya ya mamlaka yake na mahakama ya juu zaidi nchini Afrika Kusini.
Rais Zuma anasema nia yake kuu ya kuitisha uchaguzi huo wa mashinani mapema ,ni kutathmini umaarufu wa chama chake cha ANC kufuatia tuhuma kuwa amepoteza uhalali wa kuiongoza taifa hususan baada ya kupatikana na hatia ya kupuuza maamuzi ya mahakama ya taifa hilo.
Zuma aliwataka wenyeji wajiandikishe kuwa wapiga kura kwa wingi iliwathibitishie upinzani kuwa kweli Afrika kusini imekomaa kidemokrasia.
SHARE

Unknown

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment